Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 7 2022-11-01

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwandiga – Chankele – Mwamgongo hadi Kagunga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Assa Nelson Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mwandinga – Chankele- Mwamgongo hadi Kagunga yenye urefu wa kilometa 65 ni barabara ya wilaya. TANROADS wanaendelea kuifungua kutoka njia panda ya Chankele hadi Kagunga kilometa 47 na tayari kilometa nane zimeshafunguliwa.

Mheshimshiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi bilioni 1.85 kuendelea kuifungua barabara hii kwa kiwango cha changarawe. Baada ya kuifungua barabara yote, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.