Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya ajali zinazosababishwa na bodaboda kwa kutoa sight mirror?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa taarifa aliyoitoa Mheshimiwa Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza ningependa kujua TANROADS pamoja na polisi wanashirikiana vipi ili kuweka usalama wa raia barabarani?

Mheshimiwa Spika, la pili, baadhi ya bodaboda, pamoja na wapakia wateja wao wanapopita barabara huwa hawavai helmet.

Je, Wizara yako inaangalia vipi sheria wakati askari wa barabarani hawawajibiki na kutenda majukumu yao wakati wanatembea watu bila helmet?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fakharia Shomar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, namna tunavyoshirikiana na TANROADS kudhibiti usalama barabarani ni pamoja na kuimarisha miundombinu, ambayo ni shughuli ya TANROADS kwa pande barabara kuu za mikoa na barabara kuu za kitaifa, lakini kwa upande wa TAMISEMI ni TARURA, na hawa wote ni wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabara. Na Naibu Waziri, wa Wizara yenye dhamana na uchukuzi ni Makamu Mwenyekiti wakati ni Naibu Waziri Mambo ya Ndani ni Mwenyekiti. Kwa hiyo tuna ushirikiano mkubwa sana kuhakikisha kwamba kwa pamoja inapotokea ajali tunafanya uchunguzi kujua sababu na kama sababu ni za kimiundombinu, TANROADS wanahusishwa, kama sababu ni za kisheria basi polisi kwa maana ya Wizara ya Mambo ya Ndani inachukua hatua.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, bodaboda kutokuvaa helmet, hili nalo ni moja ya makosa ambayo vyombo vyetu vya usalama barabarani hususan askari wa usalama barabarani traffic police wanawaelimisha hawa vijana wanaoendesha bodaboda mara kwa mara kwa sababu kwa kweli kutovaa kofia ngumu ambazo ndizo zinaitwa helmet ni chanzo kikubwa cha vifo ambavyo vijana wetu wanaoendesha bodaboda wanapata. Kwa sababu wanapogongwa au kichwa kikigonga barabara ya lami hupasuka, au kinapogongwa na chombo kingine ama gari na kadhalika. Kwa hivyo, kuepusha madhara mkubwa haya tunawahimiza wazingatie sheria pamoja na kuvaa hii helmet.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya ajali zinazosababishwa na bodaboda kwa kutoa sight mirror?

Supplementary Question 2

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa maelezo ya Mheshimiwa Waziri, na kwa changamoto za matumizi ya barabara kwa bodaboda kuongezeka na kuhatarisha Maisha kila siku; sasa Serikali haioni leo kutoa tamko kwamba bodaboda wote wanaopita kwenye taa nyekundu, no entries pamoja na kupakia mishikaki wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimba Abbas kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ni kosa kubwa sana si bodaboda tu hata magari kukatisha wakati taa nyekundu zimewaka, zikawazuia kwenda wao wakapita; kwa sababu wakati taa nyekundu zimekuzuia wewe za kijana zimeruhusu gari nyingine kupita. Kwa hiyo, unapojaribu kukatisha kwa kweli unajiweka kwenye hatari kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba polisi wetu wa usalama barabarni huchukua hatua, lakini mara nyingine imekuwa changamoto kwa upande wa viongozi wa kisiasa kuwatetea vijana hawa. Kwa hiyo, niombe tushirikiane sote. Elimu tunatoa, sheria huchukuliwa, lakini wote tuwe na utashi wa kisiasa, kwa maana ya mabaraza ya madiwani, ngazi zetu sisi Wabunge, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya ili wote tuzungumze lugha moja kuhusu usalama wa barabarani, hususan hawa vijana wa boda boda nashukuru sana.