Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 4 2022-11-01

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: -

Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya ajali zinazosababishwa na bodaboda kwa kutoa sight mirror?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Fakharia Shomar Khamis Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya usalama barabarani Sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, Kifungu 39 (1) inayotumika Tanzania bara, na sheria ya usafiri barabarani Sura ya 7 ya mwaka 2003, Kifungu cha 22 inayotumika Zanzibar zinatamka kuwa ni kosa kisheria kwa mtu yeyote kuendesha chombo cha moto barabarani ikiwemo gari na pikipiki bila kuwa na vifaa kamili ikiwemo sight mirrors kwani chombo hicho kitahesabika kuwa ni kibovu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatoa wito kuwa, mtu yeyote anayeendesha chombo cha moto zikiwemo pikipiki za biashara (bodaboda) kufuata sheria na kutotoa sight mirror kwenye pikipiki. Kitendo cha kutoa sight mirror ni kukiuka sheria na mhusika atapaswa kukamatwa na kutozwa faini ya papo kwa papo au kufikishwa mahakamani na chombo chake kuzuiwa hadi akirekebishe.