Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kumaliza barabara ya Manyinga hadi Madizini kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali la moja la nyongeza; kwanza nichukue nafasi hii nimshukuru sana kwa niaba ya Wananchi wa Jimbo la Mvomero, Mheshimiwa Rais na kumpongeza kwa kutupa fedha nje ya bajeti ya TARURA.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuiongezea TARURA bajeti ya matengenezo ya barabara, kwa kuwa barabara nyingi zilizoko vijijini ambako kule yanapotoka mazao ya wakulima wetu, barabara zile ni mbovu.

Je, Serikali ni lini itaongeza fedha za bajeti ya TARURA ili barabara hizi ziweze kutengenezwa vizuri na kwa wakati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Jimbo la Mvomero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ofisi ya Rais – TAMISEMI, tunapokea pongezi kwa niaba ya Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini suala la pili la msingi ni kwamba nimhakikishie tu kwamba Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais wetu kipenzi, Mama yetu Samia Suluhu Hassan inazingatia jambo hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amezungumza hapa la kuongeza bajeti kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, nimuondoe shaka tu kwamba fedha bahati nzuri iliyopo ipo na tutaendelea kuifanyia kazi na nyongeza yoyote tutaendelea kuileta kwa wananchi.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kumaliza barabara ya Manyinga hadi Madizini kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii, naomba kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga, barabara ya Maswa – Kadoto, kupitia Mnadani kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lucy Sabu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba bahati nzuri maeneo aliyoyataja yapo katika mipango yetu na kadri tutakavyoweka fedha maana yake tutayajenga na yatakamilika. Ahsante sana.