Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha kupoza umeme Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ahadi ya Wizara ya Nishati kwa kituo hiki cha kupoza umeme ambacho kinatarajiwa kujengwa kwenye Kata ya Mbutu iliyopo Jimbo la Igunga ilikuwa ifanyike kwa mwaka huu wa fedha, lakini naona Serikali wameamua kuisogeza tena mwakani; ukiangalia imekuwa na changamoto kubwa kwa sababu tunapata umeme kutoka Lusu, Nzega ambayo ni kilometa 100. Sasa je, Serikali haioni kuchelewa kujenga kituo hiki ni kudumaza uchumi wa wananchi wa Jimbo la Igunga?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Ngassa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatilaji wake wa mara kwa mara. Ni kweli Serikali ilikuwa imetoa ahadi ya kukijenga kituo hiki, lakini mwaka 2021 na mwaka huu wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia TANESCO imefanya upembuzi yakinifu katika maeneo yote Tanzania Bara kuona uhitaji halisi wa ujenzi wa vituo vya kupooza umeme.

Mheshimiwa Spika, naomba uniruhusu niseme kwamba upembuzi yakinifu ulipokamilika, tukabaini mahitaji kutoka maeneo mbalimbali na uhitaji wa haraka zaidi kutoka eneo moja kwenda eneo lingine. Kwa hiyo, Kituo cha Igunga hakijachelewa ila imeonekana kijengwe mwakani kwa sababu kuna wenye uhitaji mkubwa zaidi kwa mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, naomba uniruhusu nivitaje vile vituo ambavyo vitajengwa mwaka huu ambavyo tayari vimepatiwa fedha katika ule mradi wetu wa grid stabilization project.

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha kupoza umeme Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa muktadha wa hali ya umeme ya Igunga, Julai 19, Mheshimiwa Waziri akiwa Biharamulo alieleza kwamba mnamo mwezi Septemba umeme wa gridi ya Taifa utakuwa umefika Kigoma. Sasa tupo mwezi Septemba, tunataka kujua hali ya umeme wa gridi ya Taifa: Je, umeshawasili Kigoma?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Assa Makanika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, umeme wa gridi utafika Mkoani Kigoma mwezi huu Septemba kwa sababu ipo njia ya msongo kV 33 ambayo inakamilishwa mwishoni mwa mwezi huu inayotokea Nyakanazi kupita Kakonko – Kibondo Kwenda mpaka Kasulu. Kwa hiyo, umeme wa gridi kwa kuanzia utaingia mwezi Septemba katika Mkoa wetu wa Kigoma.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha kupoza umeme Igunga?

Supplementary Question 3

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kumekuwa na changamoto ya katikakatika ya umeme katika Jimbo la Igalula lakini ukiuliza, unaambiwa changamoto hiyo inasababishwa na kusafiri kwa umbali mrefu wa nishati hii ya umeme: Je, Serikali haioni haja ya kujenga vituo vya kupoozea umeme katika Kata ya Kigwa na Kizengi ili kupunguza adha ya kusafiri umeme na kupunguza changamoto ya katikakatika hii ya umeme?

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika huu mpango wa grid stabilization project kwa mwaka huu wa fedha, Tabora inavyo vituo viwili vya kupooza umeme ambacho kitajengwa pale Uhuru katika Wilaya ya Urambo na kingine kitajengwa Ipole katika Wilaya ya Sikonge. Kwa Mheshimiwa Venant kule Igalula nitaenda kuangalia kwenye mpango wetu wa ujenzi wa vituo vya kupooza umeme katika wilaya zenye mahitaji na nitamfahamisha ni lini Serikali imejipanga kukijenga katika eneo lake. (Makofi)

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha kupoza umeme Igunga?

Supplementary Question 4

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Waziri kwmaba amekitaja kituo cha kupoozea umeme Urambo: Je, anawahakikishiaje wananchi wa Urambo kwamba lini kituo hicho kinakamilika? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Margaret Sitta na wananchi wa Jimbo lake kwamba katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 kutoka katika Shilingi bilioni 500 ambazo zimewekwa kwa ajili ya uendelezaji wa gridi, vile vituo 15 vitakavyojengwa, na cha kwake cha pale Uhuru kitakamilika bila matatizo yoyote.