Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 32 2022-09-14

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha kupoza umeme Igunga?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO imebaini uhitaji wa vituo vya kupoza umeme katika Wilaya zote Tanzania Bara zenye uhitaji huo. Aidha, imeweka mpango wa ujenzi wa vituo hivyo kulingana na uhitaji kuanzia mwaka huu wa fedha 2022/2023. Kituo cha Kupoza umeme cha Igunga kitawekwa katika mpango wa ujenzi wa mwaka ujao.

Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha huduma ya umeme katika maeneo ya Wilaya ya Igunga na Nzega, Serikali inaendelea na mradi wa upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha Lusu kilichopo Wilayani Nzega kutoka MVA 15 132/33kV hadi MVA 60 132/33kV. Upanuzi huu, utakamilika ndani ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.