Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha kifedha JKT ili iweze kutekeleza kwa ufanisi mradi mkubwa wa kilimo cha mpunga Chita JKT – Morogoro na Shamba la Mngeta?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwakuwa eneo hili kuna baadhi ya maeneo tayari yana miundombinu ya umwagijiaji na miundombinu hii ipo ardhini na ikikaa kwa muda mrefu inaweza kuharibika nataka kujua: -

Je, ni lini hasa Serikali itatenga kiasi hichi cha Shilingi bilioni 11.5 ili kunusuru miundombinu hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwakuwa maeneo mengi nchini katika mikoa yetu yana madhari yanayofanana na Mngeta na maeneo ya Chita.

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati sasa wa kutengeneza miundombinu ya umwagiliaji kwa pamoja ili kupambana na uhaba wa chakula pamoja na kuendeleza usalama wa chakula nchini? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Dar es Salaam. Kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana kwa kazi nzuri anayoifanya katika mkoa wake, lakini pia kwa hamu aliyonayo ya kuona kwamba siku moja jeshi hili linazidi kusonga mbele hasa katika shughuli za sekta hizi za kilimo. Hongera sana Mheshimiwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaanza mchakato na ukweli huu unapatikana katika jibu langu la msingi; ukiangalia kwenye mstari wa mwisho, utaratibu wa ndani unaendelea ili kuwasilisha maombi ya fedha Wizara ya Fedha na Mipango. Kwa hiyo, suala hilo la upatikanaji wa hizi Shilingi bilioni 11 tayari utaratibu tumeshauanza na muda wowote tunategemea kupata hizi fedha na tukizipata tutakwenda kufanya kile ambacho Mheshimiwa ameshauri.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kweli tumegundua na utafiti unaonesha kwamba shughuli za kibinadamu zikiwemo za kilimo, mifugo, uvuvi, madini na nyingine, kwa kweli zimekuwa zinaathiri sana vyanzo vya maji, athari ambazo mwisho wa siku zinakwenda kuharibu shughuli za kilimo na kufanya shughuli hizi zisiende vizuri.

Mheshimiwa Spioka, kikubwa nimwambie Mheshimiwa kwamba tumeshakaa na tutaendelea kukaa kufanya stadi mbalimbali kwa kushirikiana na wenzetu wa Tawala za Mikoa kwa maana ya wa Halmashauri, Vijiji na wale wa Mamlaka ya Mabonde ili kuona namna ambavyo tunahuisha vyanzo vya maji kwa ajili ya kuboresha shughuli za kilimo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)