Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 31 2022-09-14

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha kifedha JKT ili iweze kutekeleza kwa ufanisi mradi mkubwa wa kilimo cha mpunga Chita JKT – Morogoro na Shamba la Mngeta?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Dar es Salaam kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa kifedha kila mwaka ili liweze kutekeleza kwa ufanisi shughuli zake, ikiwa ni pamoja na miradi ya kilimo, ikiwemo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika shamba la mpunga lililopo Chita mkoani Morogoro na Shamba la Mngeta. Katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 Serikali ilitoa Shilingi 4,000,000,000 ambazo zimetumika kununulia zana na vifaa vya kilimo kwa ajili ya shamba la Chita. Aidha, katika Mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi 4,000,000,000 katika bajeti ya maendeleo kwa ajili ya kumalizia awamu ya kwanza ya ujenzi wa skimu ya umwagiliaji wa ekari 2,500 huko Chita.

Mheshimiwa Spika, Katika kuliendeleza shamba la Mngeta lenye ekari 12,000, kiasi cha Shilingi 11.5 zinahitajika kwa ajili ya ununuzi wa zana, matengenezo na maboresho ya miundombinu ya uzalishaji, na gharama za uendeshaji. Wizara inaendelea kufanya mazungumzo na Wizara ya kilimo ili kuona uwezekano wa shamba hili la Mngeta, kuwa sehemu ya mpango wa skimu za umwagiliaji. Taratibu za ndani zinaendelea ili kuwasilisha maombi ya fedha Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.