Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwanunulia mitambo ya kisasa na kuwapa mikopo wanawake ambao wanazalisha pombe za kienyeji?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER MICHAEL SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nimesikiliza majibu ya Serikali siyo mbaya, ni hivyo hivyo. naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba na kwamba wanatambua uzalishaji ambao upo vijijini Je, Serikali sasa haioni kwamba kuna haja ya kubadilisha Sheria ya Vilevi na Vileo (The intoxication Liquors Act) ambayo ni ya mwaka 1968 na marekebisho yake ya mwaka 1978. Hauni kuna haja; kwamba, sheria hii ikibadilishwa inaweza ikaendana na mazingira tuliyonayo sasa kwa ajili ya kuendelea kuwasaidia wananchi waliopo kule vijijini? Kwasababu Sheria iliyopo sasa hivi inaongelea sana mambo ya leseni.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kulingana na Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi kusisitiza uchumi wa viwanda Je, Wizara hii haioni sasa ipo haja kabisa ya kuwapa SIDO jukumu la kuwasaidia wananchi hawa wanawake wa vijijini na sehemu zote, kuwapa elimu, kupata takwimu halisi ili waweze kuwasaidia kuboresha hizo pombe zao za kienyeji na ziweze kuwa kwenye viwango na ziweze kuuzwa nje ya nchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester Sichalwe Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, na ninadhani ni mawazo mazuri, kwamba tuangalie namna ya kupitia sheria zetu za vileo na vilevi ili iweze kuendana na uhalisia wa sasa. Nadhani hii kama Serikali tuichukue. Na kwasababu ni wajibu wetu kama Wabunge kutunga sheria hizi basi na sisi tutalifanyia mchakato ili tuweze kuona uhalisia kama kuna uhitaji wa kubadilisha sheria hizo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kweli kupitia SIDO Serikali inaboresha baadhi ya mitambo lakini pia na kuboresha mikopo kwa ajili ya wajasiliamali mbalimbali ikiwemo wanawake. Na sasa labda tutaangalia mahsusi kwa ajili ya hawa wazalishaji wa pombe za kienyeji ambao huenda watataka teknolojia mahsusi au mfuko maalum ili waweze kuwezeshwa kuzalisha pombe ambazo zina viwando badala ya kuendelea kuzalisha hizi pombe ambazo tunaita ni za kienyeji. Nakushukuru.