Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 29 2022-09-14

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuwanunulia mitambo ya kisasa na kuwapa mikopo wanawake ambao wanazalisha pombe za kienyeji?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushuru. Kwa niaba ya Waziri wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshiniwa Condester Michael Sichalwe Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uzalishaji na uuzaji wa pombe za kienyeji unaofanyika vijijini na katika baadhi ya maeneo ya mijini. Kwa sasa Serikali haijaanzisha mpango wa kuwanunulia mitambo ya kisasa na kuwapa mikopo wanawake wanaozalisha pombe za kienyeji. Hata hivyo, wanawake wajasiriamali wataendelea kupata mikopo kupitia mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi. Nakushukuru.