Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, ni kesi ngapi za wakulima kulishiwa mazao yao zimeripotiwa na ngapi zimepelekwa mahakamani katika Wilaya ya Kilosa?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kuniruhusu kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza nikiri kwamba Serikali imefanya kazi kubwa sana Wilayani Kilosa na nimpongeze DC wa Wilaya Kilosa Alhaji Majid Ahmed Mwanga kwa kazi kubwa ya kupunguza na kuondoa kabisa katika baadhi ya maeneo migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na hayo kwa namba hizi ambazo naziona na ripoti nyingi za matatizo ya wakulima kulishiwa mazao yao katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Je, nini mkakati wa Serikali wa kumaliza matatizo haya?

Pili, Serikali haioni wakati umefika sasa wa kulichukulia jambo hili kama janga la kitaifa Wizara ya Mambo ya Ndani ikae na Ofisi ya Waziri Mkuu kuona namna bora ya kulichukulia suala hili kama janga? Nashukuru.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi na vyombo vingine vikiwemo vya Mahakama kwa kweli tumechukua hatua nyingi na tofauti, moja tumegundua kwamba bado kuna watu uelewa wao ni mdogo katika hili. Kwa hiyo cha kwanza ni kuendelea kuwapa taaluma wananchi juu ya suala hili, lakini kingine tunaendelea kutoa maelekezo kwa baadhi ama kwenye vyombo mbalimbali ikiwemo watu wa halmashauri, watu wa miji na majiji ili kuendelea kutusaidia kulilea suala hili ili kuhakikisha kwamba mambo haya yanaondoka kabisa katika jamii.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa upande mwingine nikiri kwamba kweli hili suala ni janga na kwa sababu linarudisha nyuma hali za wananchi zikiwemo hali za kiuchumi na mambo mengine kwa hiyo kutokana na hali hii ndiyo maana sasa tukaona pia bado kuna haja ya kuchukua baadhi ya mikakati na hatua hizi. Kwa hiyo nikiri kwamba hili ni janga na kwa sababu linawaathiri sana wananchi.