Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 25 2022-09-14

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je, ni kesi ngapi za wakulima kulishiwa mazao yao zimeripotiwa na ngapi zimepelekwa mahakamani katika Wilaya ya Kilosa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kesi zilizoripotiwa polisi za wakulima kulishiwa mazao yao Wilayani Kilosa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2018 hadi 2022 ni kesi 1,403. Katika kesi hizo zilizofikishwa mahakamani ni 1,037 na zilizotolewa hukumu na mahakama ni kesi 540.

Mheshimiwa Spika, vilevile kesi 356 ziliondolewa ama kufutwa mahakamani kutokana na sababu mbalimbali. Nakushukuru.