Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali katika kutatua changamoto ya wimbi kubwa la mauaji hapa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni lini sasa taarifa hiyo ya tume itawekwa wazi kwa wadau na wananchi wote kuifahamu na kuijua?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, migongano na migogoro hii imesababisha wananchi kujichukulia sheria mkononi, na je, Serikali haioni haja ya kuja na mkakati wa pamoja kama Serikali mkakati wa haraka kuhakikisha namna gani tunakabiliana na hii changamoto ya watu kujichukulia sheria mkononi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama ambavyo tumesema katika jibu letu la msingi kwamba kufuatia kuongezeka kwa matukio haya tayari Serikali imeunda tume ama timu maalum kwa ajili ya kuchunguza na kuweza kuleta majibu.

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kweli timu iliundwa na taarifa zimekuja, majibu yamekuja lakini bado Serikali tunaangalia kama kutakuwa kuna haja ya namna ya kuweza kutoa hizi taarifa kwa jamii basi zitatolewa. Kama hatuna namna basi tutaona namna nyingine ya busara zaidi ya kuwafikishia majibu wananchi ya tume hii iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza hayo matukio.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusiana na mkakati, ama bila ya shaka kuna haja ya kuwa na mkakati na mkakati upo, na mkakati wa kwanza katika hili ni kuendelea kuwaelimisha watu. Moja kuhusiana na masuala haya ya kishirikiana, kwamba si kila ambaye anakuwa na sababu hizo maana yake auliwe. Lakini kingine ni kushurutisha sheria kwamba watu lazima wafuate sheria na wasijichukulie sheria ama hatua mikononi mwao. Nashukuru.