Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 24 2022-09-14

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali katika kutatua changamoto ya wimbi kubwa la mauaji hapa nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge Wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, ni kweli kumekuwa na ongezeko la matukio ya mauaji hapa nchini. Matukio mengi yanasababishwa na wananchi kwanza kujichukulia sheria mikononi mwao, lakini pili ni wivu wa mapenzi, lakini zaidi migogoro ya ardhi, ulevi na imani za kishirikina.

Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti wimbi hili tuliunda tume maalum ya kuchunguza na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua, pamoja na kuchukua hatua za kisheria kama zilivyopendekewa na tume tuliyoiunda, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kwa kuwashirikisha viongozi wa siasa, dini, wazee wa mila na watu wanaoheshimika kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi, katika kutatua migogoro na migongano katika jamii. Nashukuru.