Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, kuanzia mwaka 2015 hadi 2020 ni fedha kiasi gani kwa ajili ya vijana, akinamama na watu wenye ulemavu zimekopeshwa na kurejeshwa?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, kwanza kutokana na majibu haya naomba nimpongeze Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Hanifa Suleman Hamza ambapo mwaka jana yeye amefanikisha kupeleka mikopo ya asilimia mia moja ya shilingi bilioni 3.1 kwa watu wa Kinondoni, nimpongeze kwa hilo.

Mheshimiwa Spika, swali langu, kwa kuwa marejesho yanaonekana hayakuwa asilimia mia moja kuna asilimia 31 ya fedha za mikopo hazijarejeshwa. Je, Serikali ipo tayari kufanya performance audit ili kuweza kujua kama fedha hizi kweli ziliwafikia walengwa na sababu ya kutokurudishwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali iko tayari kufanya utafiti kujua kwamba fedha hizi zinapopelekwa kwa walengwa hakika zinawafikia na zinabadilisha Maisha yao kiuchumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika kipindi hiki cha miaka mitano marejesho yalikuwa asilimia 69.32 na Serikali ilifanya performance audit kwa kuhakikisha kwamba tunaita halmashauri zote 184 na kuona mtiririko wa mikopo kwa miaka yote mitano.

Mheshimiwa Spika, maelekezo tuliyoyatoa Serikali ni kuhakikisha tunabainisha vikundi vyote ambavyo vilikopeshwa na vilikuwa havikurejesha marejesho hayo na virejeshe marejesho hayo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari marejesho yanakwenda vizuri, kwa vikundi vyote ambavyo vilikopa na vilikuwa havijarejesha.

Mheshimiwa Spika, pili, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwanza tumeanzisha mfumo wa kielektroniki wa kikopeshaji wa mikopo wa asilimia kumi, na halmashauri zote zimelekezwa kuingiza vikundi vyote vilivyokopeshwa na ambavyo havijarejesha kwenye mfumo wa kielektroniki ambao tutaufutilia kila siku na kuona kila hatua ya marejesho ya fedha hizo. Kwa hiyo, mpango huu wa asilimia kumi umeboreshwa kwa kiasi kikubwa na marejesho yanakwenda vizuri. Ahsante.