Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 22 2022-09-14

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, kuanzia mwaka 2015 hadi 2020 ni fedha kiasi gani kwa ajili ya vijana, akinamama na watu wenye ulemavu zimekopeshwa na kurejeshwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutoa mikopo inayotokana na asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazosimamia mikopo hiyo.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2015 hadi mwaka 2020 Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ilitoa mikopo ya jumla ya shilingi bilioni 133. Katika kipindi hicho jumla ya shilingi bilioni 92.21 sawa na asilimia 69.32 zilirejeshwa kutoka kwa vikundi vya wanufaika.