Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kueneza matumizi ya TEHAMA katika kufundisha ili kuwaokoa walimu na matatizo ya mgongo na shingo?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA H. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwanza nimwambie tu Mheshimiwa Waziri kwamba hivyo vishikwambi ambavyo vimetumika kwenye sensa havitaweza kutosha kwa walimu wa nchi nzima kwa sababu waliokuwa wanahesabu sensa na idadi ya walimu ni tofauti kabisa. Sasa: Je, mna mpango gani wa kuhakikisha mnaongeza vifaa na kuweka projector kwenye kila shule ili kuondokana na suala la magonjwa na shingo na mgongo kwa walimu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Mmetoa mafunzo kwa walimu ambao watakwenda kufundisha wanafunzi: Je, mmewaandaa namna gani hawa wanafunzi wanaokwenda kufundishwa kwa sababu somo hili litakuwa ni jipya kwao hasa kwenye maeneo ya vijijini? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Subira Mwaifunga Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimeeleza katika majibu yangu ya msingi kwamba vishikwambi vilivyotumika katika zoezi la sensa ni zaidi ya 205,000 lakini sisi kama Wizara tumeongeza vishikwambi vingine zaidi ya 100,000. Kwa hiyo, nimwondoe hofu kwanza. Idadi ya vishikwambi ambavyo wizara imeweza kuratibu na kununua vitatosheleza kwa walimu wote.

Mheshimiwa Spika, niongezee hapo katika swali lake lingine ambalo anazungumzia habari ya kuwaandaa wanafunzi na vilevile kuandaa walimu. Serikali inaendelea na mchakato wa kuhakikisha kwamba tunakuwa na vifaa toshelezi katika maeneo yote na hata katika bajeti yetu ya mwaka huu 2022/2023 tumeweka fungu kwa ajili ya ununuzi wa vifaa, lakini tutaanza kwanza na kuimarisha vituo vile vya kufundishia walimu, zile TRC zetu.

Mheshimiwa Spika, vituo vile vyote 162 tayari tumevikarabati, tumenunua vifaa pamoja na projector katika vituo hivyo kwa kuhakikisha kwanza walimu tunaweza kwenda kuwafundisha wakiwa kule kule makazini pamoja na uwepo huu wa vishikwambi, itakuwa ni rahisi kuwafundisha.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hiyo, Serikali ipo katika mpango wa kuandaa maktaba mtandao ambapo tunaamini maktaba hii itakapokamilika vitabu vyote vya kiada na ziada vitakuwepo kwenye maktaba hiyo na itakuwa ni rahisi kwa wanafunzi pamoja na walimu kupata mafunzo na mada mbalimbali kutoka kwenye maabara hizo. Nakushukuru sana.

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kueneza matumizi ya TEHAMA katika kufundisha ili kuwaokoa walimu na matatizo ya mgongo na shingo?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya jitihada kubwa kama ambavyo umeeleza za kuhakikisha inanunua vifaa vya TEHAMA nchini pamoja na kuwafundisha Walimu: Je, ni vipi jitihada hizi zinaunganishwa kuhakikisha kwamba tunaitumia TEHAMA kupunguza au kuondoa kabisa tatizo la upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi nchini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali lake la msingi, Serikali bado inaendelea na jitihada ya kuzalisha walimu katika masomo ya sayansi nchini. Sambamba na hilo, kama nilivyozungumza ni kwamba tunaendelea na ununuzi wa vifaa vya TEHAMA na mahali tutakapoanzia ni kwenye vituo vyetu vya TRC na lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba vifaa vile tunaweza kwenda kuwafundisha walimu wetu.

Mheshimiwa Spika, lengo kuu la kuanzisha vituo hivi ni kuhakikisha kwamba tuna-absorb walimu wengi zaidi kuweza kuwafundisha katika maeneo hayo ili watakaporudi kule shuleni waweze kufundisha, kwa sababu siyo lazima walimu wa TEHAMA watokane na wale walimu wa sayansi tu.

Tukishawafundisha walimu wetu, hata wale walimu wa masomo ya kawaida bado wanaweza kutumika katika kufundisha somo hili la TEHAMA.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kueneza matumizi ya TEHAMA katika kufundisha ili kuwaokoa walimu na matatizo ya mgongo na shingo?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa swali la nyongeza. Tunaipongeza Wizara kwa jitihada yake inayofanya kwa ajili ya TEHAMA. Kwa wale wanafunzi wanaoona watapewa vishikwambi: Je, kwa wale wanafunzi wenye uono hafifu Serikali itawasaidiaje? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada zake za kuhakikisha kwamba watoto wote wakiwemo na wale wenye uono hafifu na wenye ulemavu wa aina mbalimbali wanaweza kupata vifaa vya kujifunzia na kufundishia. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ina takwimu sahihi za wanafunzi hawa na tutahakikisha nao vilevile katika eneo hili tunakwenda kuwapatia vifaa vya kuwasaidia na wao kuweza kujifunza somo hili muhimu la TEHAMA. Ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kueneza matumizi ya TEHAMA katika kufundisha ili kuwaokoa walimu na matatizo ya mgongo na shingo?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Majibu ya Waziri yameonesha Serikali ina mpango wa kuanzisha Maktaba Mtandao lakini kiuhalisia maeneo mengi nchini hakuna mtandao na umeme. Tunataka kujua ni nini mkakati wa Serikali kushirikiana na Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia kuhakikisha kwamba program hii inafika kwa wakati katika shule zetu zote? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli anachozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna changamoto ya mtandao maeneo mengi, lakini nimwondoe hofu kwamba Serikali yetu inaendelea na uimarishaji wa mtandao kwa kujenga mkongo wa Taifa. Nasi kama Wizara tayari tuna mradi mkubwa sana ambao utahakikisha tunakwenda kuziunganisha shule zetu na mkongo huu na vilevile kuziunganisha kwenye mtandao wa internet.

Mheshimiwa Spika, mradi huu utaanza na mikoa 10 katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 na tunaamini mpaka kufika mwaka 2025 basi utakuwa umefikia mikoa yote, lakini shule zote zitakuwa zimeunganishwa na mtandao wa internet kuhakikisha kwamba masomo haya ya TEHAMA yanakwenda kufanyika mpaka kule vijijini. Nakushukuru sana.