Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 46 2022-09-15

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kueneza matumizi ya TEHAMA katika kufundisha ili kuwaokoa walimu na matatizo ya mgongo na shingo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji kuanzia mwaka 2019/2020, Serikali kupitia Programu ya Kuimarisha Mafunzo ya Elimu ya Ualimu (TESP) imeendelea kutoa mafunzo kwa wakufunzi wa Vyuo vya Ualimu kuhusu matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, katika mwaka 2021/2022 Serikali kupitia Programu ya Mafunzo Endelevu kwa Walimu Kazini (MEWAKA) imewezesha mafunzo kwa walimu wa Shule za Msingi 30,400 yanayohusu matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kugawa vishikwambi vilivyotumika katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi mwezi Agosti, 2022 kwa walimu wote nchini kwa lengo la kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji. Nakushukuru sana.