Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Wananchi wa Wilaya ya Mkoani waliosajiliwa kwa muda mrefu watapewa Vitambulisho vya NIDA?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa wananchi ambao wamejisajili mwaka 2018, 2019 na 2020 na baadhi yao mpaka leo hawajapata vitambulisho hivyo: Nini kauli ya Serikali? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Abdulrahman Mwinyi, Mbunge wa Chambani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza wakati najibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, kuhusu changamoto hii ya upatikanaji wa vitambulisho nilizungumza kwa ujumla wake na majibu yale yale yanaweza kusaidia kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Mwinyi kuhusu changamoto hii ya upatikanaji wa vitambulisho kwa nchi nzima ambayo inakumba majimbo yote likiwemo jimbo la Chambani.

Mheshimiwa Spika, nilieleza hatua gani Serikali imechukua ili kukabiliana na jitihada hizo. Hivyo basi, namwomba Mheshimiwa Mbunge aridhie na majibu yale yale ambayo nimeyajibu ambayo yaliainisha hatua ambazo Serikali inachukua kukabiliana na changamoto ya upungufu wa upatikanaji wa kadi kwa wananchi wa nchi nzima wakiwemo wananchi wake wa Jimbo la Chambani.