Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 44 2022-09-15

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: -

Je, ni lini Wananchi wa Wilaya ya Mkoani waliosajiliwa kwa muda mrefu watapewa Vitambulisho vya NIDA?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Abdulrahman Mwinyi, Mbunge wa Jimbo la Chambani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa imeandikisha jumla ya wananchi 47,557 ambayo ni sawa na asilimia 94 ya waliokadiriwa kuandikishwa katika Wilaya ya Mkoani. Aidha, Namba za Utambulisho 45,785 zilizalishwa sawa na asilimia 96 ya wananchi wote walioandikishwa.

Mheshimiwa Spika, jumla ya vitambulisho 41,494 ambayo ni sawa na asilimia 91 ya Namba za Utambulisho vimegawiwa kwa wananchi wa Wilaya ya Mkoani. Aidha, mwezi Septemba, 2022 jumla ya vitambulisho 1,000 vimepelekwa Wilaya ya Mkoani ili vigawiwe kwa wananchi. Serikali itaendelea kuzalisha vitambulisho na kuvigawa kwa wananchi walioandikishwa.