Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 1

MHE. JASEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Pamoja na majibu yake nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Kagera/Nkanda iko kilomita 70 kutoka Makao Makuu ya Wilaya. Kutoka Kagera/Nkanda mpaka Mgonde mara nyingi hutokea uhalifu wa utekaji wa magari, ikitokea dharura usiku wanawake wanashindwa kufikishwa katika hospitali ya Wilaya kutokana na kuogopa kutekwa magari usiku.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kata ya Kagera/Nkanda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba Kata hii ya Kagera Nkanda iko mbali sana kutoka Makao Makuu na ndiyo maana katika mwaka ujao wa fedha Serikali itatenga Milioni 500 kuhakikisha tunajenga kituo cha afya katika Kata hii na kuondolea wananchi changamoto ya kusafiri umbali mrefu kwenda kupata huduma za afya katika hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba katika mwaka huu wa fedha, Serikali itapeleka magari ya wagonjwa, Halmashauri hii pia itapata gari moja la wagonjwa. Kwa hiyo, sasa Halmashauri inaweza kuona namna ya kulipeleka katika eneo hili ili litoe huduma bora kwa wananchi wa Kata hiyo. Ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kata ya Kalembo, Isongole pamoja na Malangali katika Wilaya ya Ileje ni miongoni mwa Kata ambazo hazina kituo cha afya. Naomba kufahamu, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata hizo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Shonza, amekuwa mara kwa mara akiulizia kuhusiana na Kata hizi na amekuwa akiwasemea kwa dhati wananchi wa Mkoa wa Songwe. Nimhakikishie kwamba Serikali itaendelea kuhakikisha inakwenda kwa awamu na kimkakati kujenga vituo vya afya katika Kata ambazo amezitaja. Ahsante.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi ambacho kimejengwa kwa nguvu za wananchi katika Jimbo la Muhambwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Florence Samizi, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wananchi wa Kata aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge wametoa nguvu zao, wameanza ujenzi wa kituo cha Afya na Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia. Tumekubaliana kwamba tukipata fedha tutakwenda kuchangia nguvu za wananchi pale, kituo cha afya kikamilike tuanze kutoa huduma za afya. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunakwenda kutafuta fedha kwa ajili ya kazi hiyo. Ahsante.(Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 4

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii, Vituo Vya Afya cha Chihangu pamoja na Mkwedu muda mrefu havina wodi za kulaza wagonjwa.

Je, ni lini Serikali itaenda kujenga wodi katika Vituo hiyo vya Afya vilivyoko Jimbo la Newala Vijijini? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vyetu vya afya vingi havina wodi za wazazi pamoja pia na wodi za wagonjwa wengine, kama vituo hivi ambavyo Mheshimiwa Maimuna Mtanda amevitaja. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tuna mpango wa kuhakikisha vituo vyote ambavyo havina majengo toshelezi tunakwenda kujenga majengo hayo kwa awamu ili yaweze kutoa huduma bora za afya kwa wananchi.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 5

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa hii nafasi.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Kituo cha Afya cha Kata ya Msiha na Kata ya Hiyanda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshatoa maelekezo kwa Halmashauri zetu zote kuweka vipaumbele vyao vya ujenzi wa vituo vya afya katika tarafa na kata za kimkakati. Kwa hivyo kama hizi ni kata za kimkakati, nimhakikishie Mheshimiwa Hasunga, kwamba Serikali kupitia mapato ya ndani lakini kupitia fedha ya Serikali Kuu tutaendelea kuweka hatua za ujenzi ili vituo viweze kukamilika. Ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 6

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa tulishasema tumalize vituo vya afya kwenye tarafa ambazo hazina: -

Je, ni lini Serikali itajenga Vituo kwa Tarafa za Makame, Dosudosi na Kibaya ambazo bado hazina? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Wakili Olelekaita Mbunge wa Jimbo la Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, Jimbo la Kiteto lina Tarafa ambazo bado hazina Vituo Vya Afya, na Mheshimiwa Mbunge amekuwa mara kwa mara akifuatilia hili. Nimhakikishie, kwamba mpango wa Serikali ni kujenga vituo vya afya vya kimkakati katika tarafa ambazo hazina vituo vya afya, na tutakwenda pia kutoa kipaumbele katika Tarafa za Jimbo la Kiteto ahsante.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 7

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, je lini Serikali itajenga Vituo Vya Afya katika Kata za Nyamigogo, Kabindi, Kaniha, na Nyatakala Wilayani Biharamulo? Kwa sababu tuna uhitaji mkubwa wa Vituo Vya Afya katika maeneo hayo.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eng. Ezra Chiwelesa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge na uhitaji wa vituo vya afya tutakwenda kufanya tathmini na kuona uwezekano wa mapato ya ndani kujenga vituo hivyo, lakini pia kutafuta fedha Serikali Kuu kwa ajili ya kujenga vituo hivyo kama vitakidhi vigezo vile vya kujenga vituo vya afya katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 8

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Naomba kujua, je, gari la wagonjwa lililoahidiwa kwenye Kituo Cha Afya Mgeta litaenda lini kwenye kituo hicho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Boniphace Mwita Getere Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kata aliyoitaja na uhitaji wa kituo cha afya hicho tutakwenda kuona uwezekano wa kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho kama kitakidhi vigezo tulivyoweka kwa ajili ya vituo vya afya vya Kimkakati ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Kata ya Kagera/Nkanda Wilayani Kasulu?

Supplementary Question 9

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je lini Serikali itajenga Vituo Vya Afya katika Kata za Igundu, Muhura na Kitengule katika Jimbo la Mwibara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege Mbunge Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge zinahitaji vituo vya afya, na amekwisha leta kama vipaumbele vya jimbo lake. Nimhakikishie, kwamba tumekubaliana na halmashauri, kwamba kwanza waanze kutenga fedha kwa awamu kupitia asilimia arobaini ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya hivyo; lakini pia Serikali itakwenda kuunga mkono nguvu hizo kwa ajili ya kukamilisha vituo vya afya katika maeneo hayo. Ahsante sana.