Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Morogoro.

Je, ni lini Serikali itahakikisha dawa zote zinazohitajika kwenye wodi za kinamama na vipimo vyote zinapatikana?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Kituo cha Afya cha Mkoani Ruvuma, Wilaya ya Songea, Kata ya Ruvuma, kumekuwa na tatizo la Madaktari na Matabibu ambao ni wachache sana hawakidhi kutoa huduma ya afya ipasavyo.

Je, ni lini Serikali itaongeza Madaktari na Matabibu kwenye kituo cha afya hiki ili huduma sahihi ziendelee kutolewa? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, tumeendelea kuboresha upatikanaji wa dawa lakini pia vitendanishi na vifaa tiba katika vituo vyetu. Katika kipindi cha mwaka huu fedha nyingi zimetengwa kwa ajili ya kununua vifaa tiba, Bilioni 69.95 kwa ajili ya kununua vifaatiba katika Vituo vya Afya 530 nchini kote.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha uliopita, bajeti ya dawa imeongezeka na mwaka huu wa fedha bajeti ya dawa imeongezeka. Kwa hiyo, nimhakiksishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imedhamiria kuhakikisha inaondoa changamoto ya upungufu wa baadhi ya dawa kwenye Wodi za Wazazi lakini kwenye vituo kwa ujumla lakini kuboresha huduma za vipimo vya maabara.

Mheshimiwa Spika, pili, kuhusiana na Kituo cha Afya katika Kata ya Ruvuma juu ya uchache wa Madaktari na Matabibu, Serikali imeendelea kuajiri watumishi, mtakumbuka mwisho mwa mwaka uliopita watumishi wa afya zaidi ya 7,000 wameajiriwa na kupelekwa nchini kote, zoezi hili ni endelevu tutaendelea kuajiri kwa kadri ya upatikanaji wa fedha ili watumishi hawa watoe huduma bora za afya katika vituo.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanzisha huduma za upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mafiga, Mkoani Morogoro Manispaa? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, vituo vya afya vikijengwa vinajengwa na majengo ya upasuaji na dhamira ya Serikali ni mara tu majengo ya upasuaji yakikamilika huduma za upasuaji zianze. Kwa hiyo, kama Kituo hiki cha Afya, Mafiga, jengo la upasuaji limekwishakamilika, naelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro waanze huduma za upasuaji haraka iwezekanavyo, lakini kama kituo hakijakamilika wakamilishe na baada ya hapo wasajili ili huduma za upasuaji ziweze kuanza. Ahsante. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itarekebisha au kupunguza bei ya huduma ya upasuaji hasa ya uzazi katika hospitali za rufaa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha inatoa huduma ambazo zinaendana na gharama kwa maana ya kupunguza gharama za matibabu na hasa eneo la upasuaji. Katika hospitali za Rufaa za Mikoa, bado gharama za upasuaji ni changamoto na tumekubaliana na Wizara ya Afya, pia katika maeneo ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Vituo vya Afya na hospitali za Halmashauri, bado gharama za upasuaji ni kubwa. Kwa hiyo, tunapitia lakini baada ya muda tutatoa gharama ambazo zitakuwa zinafikika kirahisi kwa wananchi wetu. Ahsante.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Napenda kuiuliza Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa jengo la x-ray katika Kituo cha Afya Inyecha, kwa sababu Serikali imeshaleta mashine ya x-ray na wananchi kwa nguvu zao wamejenga hadi hatua za boma.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha jengo hilo la x-ray?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Chikota, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imekwishapeleka mashine ya x-ray katika Kituo hiki cha Afya cha Inyecha, lakini jengo lile halijakamilika tumekubaliana na Halmashauri, kwanza watenge fedha kwa ajili ya kukamilisha jengo hilo, pia Serikali itaona namna ya kuongeza nguvu ili kukamilisha jengo hilo na kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Je, ni lini Serikali italeta mashine ya ultra sound kwa ajili ya wanawake wajawazito katika Hospitali ya Rufaa ya Ligula? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anastazia Wambura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara, maarufu kwa jina la Ligula, iko chini ya Wizara ya Afya nasi kama Serikali tunachukua hoja hiyo kuona uwezekano wa kupeleka mashine ya ultra sound mapema iwezekanavyo. Ahsante.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana Mheshimiwa Spika, nauliza ni lini Zahanati ya Mdunduwaro – Songea Vijijini itamalizika ili wananchi wale wapate huduma, toka 2014?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ntara, amekuwa akifuatilia sana suala la Zahanati ya Mdunduwaro nami nimekwisha wasiliana na Watendaji mara kadhaa tukiwa nae na ujenzi unaendelea vizuri hatua za ukamlisha. Tulishakubaliana, ifikapo Septemba, mwisho mwaka huu Zahanati ya Mdunduwaro itaanza kutoa huduma. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, kuhakikisha kwamba zahanati hii inakamilika mwisho mwa mwezi Septemba, ianze kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.