Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2022-09-15

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Wodi za Wazazi nchini pamoja na kuongeza huduma hizo kwa Wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kati ya mwaka 2018/2019 mpaka sasa, Serikali imejenga Hospitali mpya za Halmashauri 127 kati ya hizo Hospitali 70 zimeshasajiliwa na kuanza kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo huduma za dharura, upasuaji na wodi za Wazazi.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho, Vituo vya Afya 822 vimekarabatiwa na kujengwa ambapo kati ya hivyo 476 vinatoa huduma za dharura, upasuaji na wodi za wazazi. Wodi za Wazazi zimeboreshwa kwa kuweka maeneo yote muhimu kwa huduma za uzazi salama.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 12.5 kwa ajili ya kujenga hospitali 25 zitakazokuwa na Wodi za Wazazi.