Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mpango gani kuboresha The National Herbarium of Tanzania Arusha ili kuimarisha huduma za utafiti na uhifadhi wa Mimea nchini?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza: Kwa kuwa Herbarium ya TPRI, Arusha ni kituo muhimu cha uhifadhi na utafiti: Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kuajiri na kuzalisha wataalam zaidi ili kuweza kukusanya data nchi nzima badala ya ku-concentrate na mikoa miwili tu hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili: Kwa kuwa wenzetu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, hususan misitu, wana utaalamu mkubwa wa usimamizi wa Herberium: Kwa nini tusiangalie uwezekano wa kuhamisha usimamizi wa hii National Herbarium kuipeleka maliasili au angalau kuwa-engage watu wa Maliasili wakasaidiana ili kuboresha au kuongeza wigo wa uhifadhi, utafiti na utalii katika herbarium zetu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, la kuhusu kuajiri, kwa sababu, nimezungumza pale awali kwenye majibu yangu ya msingi kwamba hii tayari imeshahamia ndani ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu, ambayo tumeanza kupitia pia muundo wake na hivi sasa tunahakikisha kwamba tunawapatia nafasi pia kuweza kuajiri wataalamu zaidi kwa sababu muundo huu tunaupitia. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba na hilo pia litakuwa ni sehemu kati ya priorities kuhakikisha kwamba, tunakuwa na wataalamu wa kutosha katika eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusu kuhamisha, jambo hili lipo kisheria na hivyo linahitaji marekebisho ya sheria, lakini tumepokea kama Serikali hoja ya Mheshimiwa Mbunge. Nakushukuru sana.