Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 67 2022-09-16

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, kuna mpango gani kuboresha The National Herbarium of Tanzania Arusha ili
kuimarisha huduma za utafiti na uhifadhi wa Mimea nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, The National Herbarium of Tanzania ilianzishwa kwa Sheria ya TPRI ya Mwaka 1979. Ili kuimarisha utendaji wa Taasisi za Wizara, Serikali imeunda Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA) iliyoanzishwa kwa Sheria Na. 04 ya Mwaka 2020 kwa kuunganisha Sehemu ya Afya ya Mimea iliyokuwa chini ya Wizara ya Kilimo na Mamlaka ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kitropiki (TPRI).

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha The National Herbarium of Tanzania na kuimarisha Huduma za Utafiti na Uhifadhi wa Mimea, Serikali imepanga kuendeleza kuimarisha kanzidata ya mimea ya Tanzania inayohifadhi sampuli kavu ndani ya National Herbarium of Tanzania (NHT) pale Arusha, Mweka, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine na TAFORI. Aidha, Serikali kupitia TPHPA inaendelea Kuorodhesha, kukusanya na kutambua sampuli za mimea katika misitu ya hifadhi nne ambazo ni Mlima Hanang, Chenene, Salanga na Chemichemi, katika mikoa ya Manyara na Dodoma.