Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, Serikali inaweza kuongeza uhai wa paspoti za muda wanazopewa Madereva hadi kufikia Miezi sita?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali na kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sekta ya uchukuzi ina mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi yetu na madereva ndio wahusika wakubwa: Je, Serikali haioni umuhimu wa kuleta mabadiliko haya ya sheria ili hili kundi maalum likapata hizo hati za dharura walau kwa muda wa miezi sita hadi mwaka mmoja? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa kupata Passport ni mchakato unaochukua siku kadhaa; je, Serikali iko tayari kuwa na dawati maalum kwa ajili ya kuwahudumia madereva ambao wako tayari kupata Passport za kudumu wapate huduma kwa haraka? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu maswali mawili nya nyongeza ya Mheshimiwa Chumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli upo umuhimu wa hawa madereva kuwa na passport, lakini kwa sababu mchakato wa kutoa Passport kwa maana ya kuongeza muda wa Passport za dharura kuzidi mwezi mmoja uliopo sasa unahitaji mchakato wa mabadiliko ya sheria, ni ushauri wetu; kwa sababu hizi safari wanazifanya mara kwa mara, hakuna sababu za kwa nini wasipate hizi passport. Akiipata Passport kwa miaka 10 watakuwa wanazitumia hizi passport. Kwa hiyo, huenda kukawa na nafuu kuliko kupata Passport za dharura mara kwa mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kwa sababu ya kujua umuhimu wa madareva na safari zao, Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Idara ya Uhamiaji imeweka dirisha maalum la kuwahudumia madereva hawa ili pindi wafikapo wasikae foleni muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.