Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 64 2022-09-16

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, Serikali inaweza kuongeza uhai wa paspoti za muda wanazopewa Madereva hadi kufikia Miezi sita?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Pasipoti za muda wanazopewa madereva ni hati za dharura za safari (Emergency Travel Documents) ambazo kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Safari ya Mwaka 2002, hutolewa kwa safari moja kwa muda ulioainishwa ndani ya hati husika. Aidha, hati hii ya safari hutolewa kwa waombaji wenye safari za dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa suala la kuongeza muda wa hati za dharura za safari litahitaji mabadiliko ya sheria endapo itaridhiwa, Serikali inawashauri madereva kuomba pasipoti ili kuepuka usumbufu wa kuomba hati za dharura za safari mara kwa mara kwa vile safari zao siyo za dharura. Nashukuru.