Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, ni lini serikali itakamilisha ujenzi wa bandari zilizopo Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali imejipanga kupanua bandari za Mwanza na Bandari zile za Nansio; je, Serikali imechukua hatua gani za haraka kuhakikisha wanakamilisha hizo bandari ili ziweze kuwasaidia wananchi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Serikali imekamilisha ujenzi wa Bandari ya Karema na tayari ilishaanza kufanya kazi; je, ni lini Serikali itaanza kuleta meli kwenye eneo la Bandari ya Karema, meli za kimataifa na meli za ndani? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali imekuwa ikipanga fedha katika bajeti mbalimbali hususan kupitia TPA kwa bandari hizi za Mwanza, Nansio, Mwanza Kusini na Mwanza Kaskazini. Na hivi navyosema Bandari ya Nansio tayari tumeshafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni pamoja a Bandari za Bukoba pamoja na Kemondo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusiana na meli za Kwenda kwenye bandari yetu ambayo imezinduliwa hivi karibuni na hususan katika Ziwa Tanganyika, tunataraji hivi karibuni tutafanya mkutano na washirika ambao ni wadau muhimu katika usafirishaji wa bandari za Ziwa Tanganyika kutoka Congo, Zambia, Rwanda na Burundi. Kwa hiyo hivi karibuni utaanza kuona meli zikienda katika bandari hiyo mpya ya Kalema. Ahsante.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, ni lini serikali itakamilisha ujenzi wa bandari zilizopo Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Bandari ya Nansio ina hali mbaya na inaweza kuleta matatizo muda wowote, Mheshimiwa Waziri uko tayari baada ya Bunge hili utembelee Jimbo la Ukerewe ili uone umuhimu wa kuharakisha matengenezo ya bandari ile ya Nansio? Nashukuru.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nipo tayari mara baada ya Bunge wiki ijayo tutembelee bandari hii ya Nansio na kujionea; na nitaambatana na wataalam ili washauri vizuri zaidi. Ahsante.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, ni lini serikali itakamilisha ujenzi wa bandari zilizopo Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Ningependa kufahamu, ni lini Serikali inatarajia kujenga vituo vya kupumzikia abiria na mageti ya kushushia abiria kwenye vituo vya Kilondo, Lupingu na Manda?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika Ziwa Nyasa tumeshafanya upembuzi yakinifu katika Bandari za Nyasa pamoja na Mbamba Bay. Kwa hiyo katika mwaka huu wa fedha tumetenga fedha kwa ajili ya kuanza kujenga katika maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge.