Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 62 2022-09-16

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: -

Je, ni lini serikali itakamilisha ujenzi wa bandari zilizopo Mkoa wa Mwanza?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imekuwa ikiboresha miundombinu ya Bandari za Mwanza Kaskazini na Kusini kwa kutumia bajeti zinazopangwa kila mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, TPA imekamilisha uboreshaji wa jengo la abiria, awamu ya kwanza na matenki manne ya kuhifadhia mafuta katika Bandari ya Mwanza Kaskazini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka fedha 2022/2023 Serikali kupitia TPA imepanga kufanya utanuzi wa eneo la maegesho ya meli (berth extension), kuongeza kina cha maji (dredging) barabara ya kuingia Bandarini na kuboresha miundombinu saidizi katika bandari ya Mwanza Kaskazini. Kwa upande wa Bandari ya Mwanza Kusini, TPA imepanga kuongeza eneo la maegesho ya meli (berth extension), barabara ya kuingia Bandarini na uboreshaji wa Miundombinu saidizi. Aidha, uboreshaji huo utaenda sambamba na ununuzi wa mitambo ya kuhudumia mizigo bandarini. Ahsante.