Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni zipi sababu za Kiwanda cha Pamba na Mafuta cha Kasamwa kusimamisha uzalishaji kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. CONSANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliahidi kwamba baadhi ya viwanda vitafufuliwa kwa ubia wa ushirika na mifuko ya jamii. Sasa ninataka kujua ahadi hiyo imefikia wapi.

MheshimiwaNaibu Spika, swali langu la pili, hivi karibuni nchi yetu ilikumbwa na uhaba mkubwa wa mafuta ya kupikia. Malighafi ya mafuta ya kupikia ni pamba ambayo ipo nyingi kwenye eneo hilo.

Je, ni mkakati gani sasa ambao Serikali inao kuhakikisha kwamba kiwanda hicho kinafanya kazi? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Constantine Kanyasu Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni kweli, ni jitihada ya Serikali kuona viwanda vyetu vinafanya kazi/vinafufuliwa moja ya kimkakati ilikuwa ni kuhusisha mifuko yetu ya jamii kuona nayo inashiriki katika kuzalisha au kufufua kiwanda hiki cha Kasamwa, lakini kutokana na stadi iliyofanywa na wenzetu wa NSSF ilionekana kwamba wakati ule bado haina tija kwa wao kuwekeza kulingana na malengo ya mifuko hii ya jamiii. Kwa hiyo, hilo bado linafanyiwa kazi kuona kama kutakuwa na tija ili kuwekeza katika kiwanda hiki cha Kasamwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili mkakati wa Serikali ni kweli, moja ya maeneo ambayo Serikali imeweka mkazo ni kwenye sekta ya kilimo kuona tunaboresha kilimo ili tuwe na malighafi muhimu kwa ajili ya kuzalisha mafuta ya kula, mojawapo ni mafuta ambayo yanatokana na zao la pamba kwa maana ya mbegu za pamba. Kwa hiyo, uzalishaji utaongezeka na hivyo tunaamini viwanda hivi moja ya changamoto ilikuwa ni malighafi kwa hiyo vitakwenda kupata malighafi, ambayo itatumika pia kuzalisha pamoja na bidhaa nyingine na mafuta ya kula ambayo yanatokana na mbegu za pamba. Ninakushukuru.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni zipi sababu za Kiwanda cha Pamba na Mafuta cha Kasamwa kusimamisha uzalishaji kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Pwani unaongoza kwa zao kubwa la korosho. Je, nini mkakati wa Serikali kufufua Kiwanda cha Korosho TANITA Kibaha?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ambayo pia tunalenga katika kuhakikisha tunaongeza thamani ni kwenye zao la korosho. Viwanda vingi ambavyo vilikuwa havifanyi kazi, mkakati wa kwanza ni kuona vile inavyowezekana kurudisha katika mikono ya Serikali ili tutafutie wawekezaji wengine lakini pia pili, ni kuvutia wawekezaji wapya kuwekeza katika viwanda vipya ambavyo navyo vitaongeza kazi ya kuchakata zao la korosho ili kuziongezea thamani katika Mikoa ya Pwani na Mikoa ya Nyanda za Kusini ambao wanalima zaidi zao la Korosho. (Makofi)