Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 56 2022-09-16

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, ni zipi sababu za Kiwanda cha Pamba na Mafuta cha Kasamwa kusimamisha uzalishaji kwa muda mrefu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanda cha Pamba na Mafuta cha Kasamwa kilisitisha shughuli za uzalishaji mwaka 2012 kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo teknolojia iliyopitwa na wakati, ukosefu wa vipuri, gharama kubwa za uendeshaji hususani maji na umeme, uhitaji wa idadi kubwa ya wafanyakazi na ukosefu wa malighafi. Ninakushukuru.