Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA K.n.y. MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua Matawi ya Benki ya Kilimo katika Wilaya za Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nikijaribu kupitia huku kwenye benki hii, ni takribani miaka 10 sasa tangu benki hii ianzishwe. Ilianzishwa mwezi Septemba, 2012, lakini tunaona ina matawi matano tu. Matawi haya matano yako katika majiji haya makubwa, lakini tunajua wakulima wako kwenye vijiji vyetu na kata zetu ambako tunatoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa je, kwa sababu Serikali imesema itapanuka lakini based on kupata pesa ya mtaji mkubwa zaidi: Ni nini mpango wa Serikali kuiongezea pesa benki hii hata kupitia hazina ili wakulima wetu ambao wametutuma sisi hapa waweze kunufaika na benki hii ambayo ina miaka zaidi ya 10 lakini haijawafikia? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: tarehe 9/6/2022 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika ziara ya Mkoa wa Kagera kwenye uwanja wa Kaitaba alitoa maelekezo maalum kwa Serikali ya Mkoa wa Kagera na akai-cite kwamba tumekuwa na shida ya mafuta ya kula katika nchi hii na mpango uliopo ni kuutumia Mkoa wa Kagera ambao una maeneo makubwa ambayo hayatumiki kwa ajili ya kufanya kilimo cha michikichi na kilimo cha alizeti; na ameelekeza tutenge hekta takribani 70,000 mpaka 100,000 kwa ajili ya kutatua tatizo hili: -

Sasa je, Serikali haioni kwamba iko haja ya kuielekeza benki hii pamoja na kwamba mtaji wao bado ni mdogo, ielekee Kagera ikaungane na Serikali ya Mkoa ili waone wanasaidiaje kutatua tatizo hili la mafuta ya kula? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Eng. Ezra kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza tunalipokea kama ushauri na tunaenda kulifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili pia tunaenda kulifanyia tathmini tuone kama upo umuhimu wa kuelekea kwa wakati huu; na kwa kuwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais kunyanyua uchumi katika Mkoa wa Kagera, basi nalo hili tumelipokea na tunalifanyia kazi. Ahsante. (Makofi)