Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 84 2022-09-19

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA K.n.y. MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafungua Matawi ya Benki ya Kilimo katika Wilaya za Mkoa wa Kagera?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oliver, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki ya Kilimo (TADB) imefanikiwa kufungua matawi katika kanda tano ambazo ni Kanda ya Kati, Dodoma; Kanda ya Mashariki, Dar es Salaam; Kanda ya Magharibi, Tabora; Nyanda za Juu Kusini, Mbeya na Kanda ya Ziwa, Mwanza ambayo inahudumia Mkoa wa Kagera na wilaya zake. Aidha, Benki ipo katika hatua za mwisho za kufungua Ofisi ya Kanda ya Kusini, Mtwara na hatua za awali za kufungua Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilisha ufunguzi wa Ofisi za Kanda, TADB itaangalia uwezekano wa kufungua ofisi katika mikoa na ikiwezekana wilaya, lakini hili litazingatia uwezo wa benki wa kifedha ikiwa ni pamoja na faida na ukuaji wa mtaji. Ahsante.