Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kuleta mikataba ya madini na nishati ijadiliwe Bungeni kabla ya kuingia makubaliano na wawekezaji?

Supplementary Question 1

MHE.KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya maeneo yanayolalamikiwa katika nchi zenye utajiri wa mafuta ya gesi ni kukosekana kwa utawala bora katika kuwa na uwazi kwa mikataba hii kwa umma; je, ipi mikakati ya Serikali katika kuenzi jitihada za kufikia lengo hili la kuwa na uwazi wa mikataba kwa ujumla katika umma wa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili pamoja na kwamba mikataba imekuwa inakuja bungeni kupitia Kamati; je, Serikali haioni kama kuna umuhimu wa kubadilisha utaratibu huu ili kuwe na utaratibu ambao Bunge litaweza kuona kwa maana ya Bunge zima hata kuwe kwa kipindi cha mwisho wa mwaka ili waweze kuona ni maeneo gani ambayo Serikali imeingia mkataba na waweze kupata uelewa wa pamoja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nollo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwazi katika mikataba upo na kimsingi kwa sababu muuliza swali ni sehemu ya Wabunge na Kamati za Bunge zimeundwa kwa mujibu wa sheria na utaratibu wa Kibunge, zinapopata nafasi ya kupitia mikataba hii huwa ni kupunguza lile jambo katika mazingira ambayo yanaweza upotofu wa jumla katika suala la mikataba. Hivyo basi mikataba inapojadiliwa na Kamati za Bunge ni kisheria kabisa unakuwa tayari maelekezo yanayotolewa na Kamati zile yanakuwa ni halali na ni sawa kufikishwa mbele ya Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu lile suala la kubadilisha mfumo, ni Bunge hili lililokaa na likaweka utaratibu huo, na ni Bunge hili hili linaweza likabadilisha mfumo. Hivyo basi ni jambo ambalo ningemshauri Mheshimiwa Mbunge kutoa hoja ili sasa vyombo vinavyohusika katika kubadilisha mifumo viweze kuchukua nafasi yake. Lakini kwa namna tunavyokwenda kwa sasa ni jambo ambalo linazingatia taratibu na sheria tulizojiwekea. Ahsante.