Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 81 2022-09-19

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kuleta mikataba ya madini na nishati ijadiliwe Bungeni kabla ya kuingia makubaliano na wawekezaji?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba ya Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi Sura ya 450 kifungu cha 5 inatoa wajibu wa Bunge kwa mujibu wa ibara ya 63 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, katika utekelezaji wa jukumu lake la kuishauri Serikali linaweza kuitisha mikataba inayohusu masuala ya utajiri na rasilimali za nchi na kuweza kupitia kwa lengo la kuishauri Serikali na kutoa azimio la kuondoa masharti hasi katika mikataba. Takwa hili la sheria linazingatia misingi iliyowekwa na sheria, kwamba mikataba au makubaliano yaliyoingiwa kati ya Serikali na wawekezaji yanazingatia haki, usawa na nia njema kwa pande zote na kuzingatia maslahi ya wananchi wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiwasilisha mikataba kupitia kamati za kudumu za Bunge na Kamati kuzitolea maelekezo na ushauri kutoka kwa sekta husika. Pale Kamati husika inapoona umuhimu wa kufikisha mkataba mbele ya Bunge lako Tukufu maelekezo hutolewa na kwa kuzingatia Sheria husika.