Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, ni kwa nini wakulima wasianze kujua bei ya kuuzia tumbaku na bei ya pembejeo kabla ya kufunga mkataba wa uzalishaji?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nimuulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya kuuzia tumbaku ni muhimu sana kwa mkulima; je, wakulima wenyewe wanashirikishwaje katika kufikia uamuzi wa bei gani tumbaku yao iuzwe?

Swali la pili tunaishukuru Serikali kwa kutupa ruzuku, lakini naomba Serikali ituhakikishie sisi watu wa Urambo; je, mbolea ya tumbaku ni miongoni mwa mbolea zilizopata ruzuku? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ushiriki wa wakulima, kwa mujibu wa Sheria ya Tasnia ya Tumbaku Namba 24 ya mwaka 2021 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2009 na kanuni zake za mwaka 2011 Kifungu cha 43 (1) kimeweka masharti ya ushiriki wa wakulima kupitia vyama vyao vikuu katika majadiliano ya bei na pembejeo. Hivyo, nidhahiri kwamba kupitia sheria hii wakulima wanashiriki kupitia vyama vyao vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu mbolea ya ruzuku; katika mwongozo ambao tumeutoa kwenye mbolea ya zuruku, mbolea ya ruzuku ni kwa mbolea zote ikiwemo mbolea ambazo zinahusiana na zao la tumbaku. Kule kwenye tumbaku wanatumia mbolea hasa za NPK na CAN ambapo hadi hivi sasa kwa mujibu wa maoteo ni jumla ya tani 37,000 zitahitajika na tayari zipo kwenye utaratibu huo kuingia kwenye suala hili la ruzuku.