Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 77 2022-09-19

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, ni kwa nini wakulima wasianze kujua bei ya kuuzia tumbaku na bei ya pembejeo kabla ya kufunga mkataba wa uzalishaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Tasnia ya Tumbaku Na. 24 ya mwaka 2001 na marekebisho yake ya mwaka 2009 na kanuni za mwaka 2011, wakulima wa tumbaku wanapaswa kufunga mikataba ya uzalishaji wakiwa wanajua bei ya kuuzia tumbaku na bei ya pembejeo za kilimo. Huu ndio utaratibu uliopo unaoendelea kusimamiwa na Serikali kupitia Bodi ya Tumbaku Tanzania. Katika msimu wa mwaka 2022/2023, tayari wakulima wamepata bei ya tumbaku na pembejeo tangu tarehe 30 Agosti, 2022. Kutokana na masoko yaliyopatikana bei elekezi imepanda kutoka Dola za Marekani 1.65 mwaka 2021/2022 hadi Dola za Marekani mbili mwaka 2022/2023 kwa kilo ya tumbaku, sawa na ongezeko la asilimia 21.