Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Vuga - Mlembule katika Mji Mdogo wa Mombo Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUM M. ZODO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Mkomazi na Kata ya Mkalamo katika Jimbo la Korogwe Vijijini ni Kata ambazo zimepitiwa na Mto Ruvu lakini Kata hizo hazina maji kabisa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanapeleka maji kwenye Kata hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mradi mkubwa wa maji wa Mwanga, Same, Korogwe ni mradi ambao unasuasua. Je, Serikali ina mpango gani wa kwenda kukamilisha mradi huo wa maji ili kuondoa adha ya maji kwa wananchi wa Wilaya ya Korogwe? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zodo kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ninapenda kumpongeza Mheshimiwa Zodo kwa ufuatiliaji mzuri kwani wakinamama lazima tusemeane na tuhakikishe tunawatua ndoo kichwani akinamama wote wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata hizi mbili alizoziongelea za Korogwe Vijijini zipo kwenye mpango, mradi huu ukishakamilika kwa awamu hii ambayo utekelezaji unaendelea awamu inayofuata Kata hizi Mbili pia zitapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mradi wa Mwanga, Same, Korogwe nimetoka huko hivi majuzi mradi ni mzuri sana na kazi zinaendelea. Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote wanaotoka kwenye maeneo ya mradi huu baadhi tuliweza kuongozana mradi ni wa mafanikio makubwa sana na unaendelea kutekelezwa na utakuwa manufaa maeneo yote ambayo unapitia.