Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 72 2022-09-19

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Vuga - Mlembule katika Mji Mdogo wa Mombo Wilayani Korogwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Mzamilu Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Tanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji wa Vuga - Mlembule ulioanza kutekelezwa mwezi Julai, 2020 ambapo utekelezaji hadi sasa umefikia asilimia 80 na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2022. Kazi zilizokamilika ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake), ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji mita za ujazo 500, ujenzi wa matanki punguza mawili (2) na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa Kilometa 10.2.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zinazoendelea ni ujenzi wa matanki punguza manne (4) na ulazaji wa mabomba ya usambazaji Kilometa 4.3. Kukamilika kwa mradi huu kutanufaisha wananchi wapatao 21,284 wa Vijiji vya Mlembule, Mwisho wa Shamba, Mombo na Jitengeni.