Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawalipa Watumishi waliohamishiwa katika Halmashauri ya Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nasikitika kidogo kwa majibu ambayo Serikali imetoa, anakubaliana kwamba uhakiki umekamilika tangu 2015 na sasa ni miaka nane mpaka leo watumishi wale hawajalipwa hata shilingi moja. Hata hivyo, kinachosikitisha zaidi, wapo waliostaafu lakini pia wapo ambao wamekufa. Nataka kujua nini hatima ya hao waliostaafu na hao waliokufa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kulipa madai yoyote ya watumishi lazima uhakiki kujiridhisha zaidi ya shaka kwamba wanaodai wanadai kiwango halali na wanastahili kulipwa malipo hayo. Ni kweli kwamba uhakiki ulianza mwaka 2015/2016, lakini kuna dosari nyingi za madai zilionekana miongoni mwa wale ambao walitakiwa kulipwa na Serikali isingeweza kuwalipa kabla ya kujiridhisha kwamba kiasi ambacho wanadai wanatakiwa kulipwa. Kwa hiyo, baada ya Mkaguzi wa Ndani kutoka Makao Makuu kufanya ukaguzi, ikaonekana madai yale yameshuka na ndiyo maana yamechelewa kuanza kulipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka ujao inatengwa fedha, lakini kila mwaka tutatenga fedha kuhakikisha wote waliostaafu, walioko kazini na hata ambao wametangulia mbele za haki wanalipwa kwa kupitia wale ndugu ambao ni wategemezi wa hao waliotangulia mbele za haki.