Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2022-09-19

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawalipa Watumishi waliohamishiwa katika Halmashauri ya Chemba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ilianzishwa rasmi tarehe Mosi Julai, 2013, baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa kugawanywa. Jumla ya watumishi 90 wa idara mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, walihamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ambao walistahili kulipwa kiasi cha Shilingi milioni 238.7 ikiwa ni stahiki zao za kiutumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ilihakiki madeni ya watumishi hao na kuwasilisha Serikali Kuu maombi ya kulipwa madeni hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba katika mwaka wa fedha 2023/2024, itatenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya kulipa madeni hayo. Aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha katika bajeti za kila mwaka ili kuendelea kulipa madeni hayo.