Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kurahisisha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini ni lini hasa Serikali itaanza kugawa vitambulisho vya Taifa kwa wale ambao wameshasajiliwa hasa waliosajiliwa zaidi ya miezi sita ama zaidi ya miaka miwili? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Ninafahamu Bungeni hapa tumesema tumejadili changamoto ya Vitambulisho vya Taifa tukaeleza, lakini tukasema changamoto ile imeshakwamuliwa baada ya ku-review ule mkataba na kuuhuisha, tukasema kinachosubiriwa ni mzalishaji kuanza kutengeneza vitambulisho hivi. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge ni kweli wananchi ambao kwa miezi Sita iliyopita wamesajiliwa na kutambuliwa na wakapewa namba baada ya Mkandarasi kuanza kuzalisha vitambulisho hivyo watapewa kipaumbele watu hawa ambao wamekaa muda mrefu bila kupewa kadi zile za vitambulisho. Ninashukuru. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kurahisisha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ninataka kujua Serikali ina mkakati gani wa kuboresha vitambulisho hivi vya Taifa ili viweze kubeba taarifa muhimu zote za mhusika?(Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli baada ya kuanza kutumika kwa Vitambulisho vya Taifa ambavyo vimeonekana vimekuwa na matumizi mengi Zaidi, imeonekana umuhimu wa kuvihuisha vitambulisho hivyo ili vibebe taarifa nyingi na kumpunguzia Mtanzania utaratibu wa kubeba vitambulisho hiki, Leseni na nini. Tunaendelea kuzungumza na wenzetu wa mamlaka nyingine ambazo zina vitambulisho hivyo ili kuweza kuhuisha Kitambulisho hiki cha Taifa kiweze kubeba taarifa hizo kumpunguzia mwananchi kuwa na makadi au vitambulisho vingi. Kwa hiyo, mazungumzo yatakapokamilika Mheshimiwa Esther jambo hilo litafanyika. Ninakushukuru sana. (Makofi)