Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 93 2022-09-20

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kurahisisha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la Serikali ni kuhakikisha watu wote wanaokidhi vigezo vya usajili na utambuzi wanasajiliwa kwa urahisi. Ili kufikia lengo hilo, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inatekeleza mikakati ifuatayo: -

(i) Kufungua ofisi za usajili na utambuzi katika Wilaya zote Tanzania Bara na Zanzibar, ambapo jumla ya ofisi 152 zimefunguliwa katika Wilaya 150;

(ii) Kuendelea kufanya usajili na utambuzi wa wananchi kupitia ofisi za Mamlaka za Wilaya na kuendesha mazoezi ya usajili wa watu wengi (Mass registration); na

(iii) Ugawaji vitambulisho kwenye ngazi za msingi yaani Kata/Shehia na vijiji ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati hiyo husaidia kupunguza usumbufu na gharama za usajili kwa wananchi. Nashukuru.