Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly Ntate, nipende kuuliza swali la nyongeza – na kwanza ninashukuru kwa majibu ya Serikali – kwamba sasa baada ya kukamilisha kituo hicho, ni lini sasa watumishi wataletwa ili kuimarisha hali ya usalama katika maeneo hayo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru baada ya kituo hiki kukamilishwa nampa assurance Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly kwamba Serikali kupitia Jeshi la Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, mara moja watapelekwa Askari kwa ajili ya kuanza kutoa huduma. Ikumbukwe kwamba sasa hivi tunao Askari mpaka ngazi ya Kata na eneo hili lipo kwenye utawala wa Kata na Inspectors wameshapangwa kule wameshapangwa kule kwa ajili ya kutoa huduma za ulinzi. Kituo kikikamilika tutapeleka askari wa kutosha ili kutekeleza majukumu ya usalama kwenye eneo hilo. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunajua usalama ulivyo, Kituo cha Polisi Mgeta ni kituo kiko Makao Makuu ya Tarafa ya Chamuriho, toka mwaka jana nimeahidiwa kwamba fedha zitakwenda kumalizia boma la kituo hicho Waziri wa Mambo ya Ndani alishaahidi, wewe Naibu Waziri ulishaahidi. Je, ni lini hela zitakwenda kwenye kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumjibu Mheshimiwa Getere kwamba ni kweli kwamba kwa mara kadhaa tumeahidi kwamba kituo hicho kitakamilishwa na ndiyo tumeanza tu Mheshimiwa Getere, ni mwezi wa tatu tangu tulipoanza utekelezaji wa bajeti, ninakuahidi tu katika robo inayokuja tutahakikisha kupitia Jeshi la Polisi fedha inapelekwa ili kukamilisha ujenzi wa kituo cha Mgeta ambacho ni muhimu sana kwa usalama wa wananchi wa eneo la Mgeta na Tarafa nzima ya Wilaya ya Bunda Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.(Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kituo cha Polisi cha Sumbawanga Mjini ni cha toka enzi za mkoloni.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo hicho? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Mbunge kwamba vituo vyote ambavyo ni chakavu, wakati fulani tuliwahi kusema hapa Bungeni vimefanyiwa tathmini na kinachosubiriwa ni upatikanaji wa fedha tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele kikubwa tulikielekeza kwenye maeneo ambayo hayakuwa na vituo vya Polisi kabisa, ndiyo maana ukarabati kidogo tumekuwa tukienda taratibu ili kuhakikisha wale ambao hawana huduma za usalama wa raia kabisa angalau waweze kupata. Ninakuahidi Mheshimiwa Mbunge tunajua eneo unalolitaja linakaribia kupakana na mpakani na kuna matukio mengi ya uhalifu. Kwa hiyo tutahakikisha kwamba katika mipango yetu ya ukarabati jicho linaelekezwa kwenye kituo hicho ili kiweze kufanyiwa ukarabati. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa, Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliahidi kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Galapo katika mwaka wa fedha 2022/2023. Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kazi hiyo iweze kukamilika?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Sillo kwamba mpango wa ukamilishaji wa vituo vya Polisi kwa kweli inategemea upatikanaji wa fedha. Ninafahamu wakati wa bajeti yetu iliyosomwa mwaka huu, Waziri aliainisha maeneo mbalimbali ambayo yatapelekewa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo. Ninamuomba tu Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, miongoni mwa maeneo ambayo yatapewa kipaumbele ni haya ambayo yana matukio mengi ya uhalifu ikiwemo eneo la Galapo ambalo limekuwa ni kituo kikubwa cha kibiashara na tutakipa pia kipaumbele. Ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Supplementary Question 5

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Lukozi Wilaya ya Lushoto ni moja ya Kata kubwa yenye idadi kubwa ya watu na mwingiliano mkubwa wa kibiashara lakini kata hiyo haijapata kabisa huduma ya Polisi.

Je, ni lini sasa Serikali itaanzisha Kituo cha Polisi kwenye Kata hiyo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Husna, Mbunge wa Viti Maalum Tanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kipaumbele chetu ni kuhakikisha kwamba Kata zote zinapata huduma za Polisi hususan Polisi Shirikishi. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka uliopita tulieleza bayana, kwamba watumishi wapya Askari, Inspectors zaidi ya 4,200 waliopatikana wamepangwa kwenye Kata zote ili kuimarisha huduma za ulinzi. Ninamuomba Mheshimiwa Mbunge kupitia Halmashauri ya Wilaya Lushoto wawahamasishe wananchi waanze angalau zile shughuli za awali za ujenzi wa kituo hicho ili Serikali ije iunge mkono nguvu zao kukamilisha ujenzi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wale ambao wameweka kipaumbele na wakaanza ujenzi Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Polisi inawaunga mara moja mkono, lakini wale ambao wanataka Wizara ianze moja, uwezekano huo hautakuwepo kutokana na changamoto ya kibajeti. Nimuombe tu tuvianzishe na Wizara tutaunga mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru. (Makofi)