Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 92 2022-09-20

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: -

Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi cha Mbande ambacho ni cha Daraja B kilianza kujengwa kwa kutumia Shilingi 16,000,000 zilizochangwa na wananchi mwezi Agosti 2016. Kwa kutumia Shilingi 38,000,000 zilizochangwa na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mradi wa SONGAS na Kampuni ya Tatu Mzuka ujenzi uliendelea hadi upauaji mwaka 2020.

Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi, ilitoa Shilingi 30,826,500 mwezi Juni, 2022 ili kuendeleza na kukamilisha ujenzi huo. Hadi sasa milango, grills za madirisha, mfumo wa majisafi na majitaka, umeme na blundering vimekamilishwa. Ni matarajio yetu kuwa Kituo hicho kitakamilika na kuanza kutumika kabla ya mwezi Novemba, 2022. Ninakushukuru.