Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini mifuko ya kuwezesha wananchi kiuchumi itaunganishwa ili kuleta tija na manufaa kwa Watanzania hasa waishio vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali ilitueleza kwamba kuna viwanda vya kuanzia 3,500,000 na katika Mkoa wetu wa Kagera kina mama wamekuwa wakikopeshwa mikopo isiyo na tija.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwakopesha hivyo viwanda badala ya pesa ili kutengeneza ajira nyingi mkoani kwetu Kagera? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Kagera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akifatilia sana kuhusiana na wafanyabiashara wakina mama wajasiriamali katika Mkoa wa Kagera. Nimshukuru sana kwa kazi kubwa anayoifanya Mheshimiwa Oliver. Lakini kuhusiana na mitaji hii ni kweli wajasiriamali wadogo hasa akina mama tunataka kupitia Shirika letu la Viwanda Vidogo kuwakopesha viwanda au teknolojia rahisi za kufanyia biashara zao badala ya kuwapa fedha ambazo wakati mwingine zinaweza kutumika katika malengo yasiyokusudiwa.

Kwa hiyo, moja ya mikakati ni hiyo kuwapa viwanda ili iwasaidie kuzalisha bidhaa ndogondogo pia waweze kukidhi mahitaji ambayo wameomba katika mikopo hii. Nakushukuru sana.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini mifuko ya kuwezesha wananchi kiuchumi itaunganishwa ili kuleta tija na manufaa kwa Watanzania hasa waishio vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Je, ni upi mpango wa Serikali kupitia Wizara hii ya Uwekezaji kuangalia yale makundi ya asilimia 10 ambayo hayana vigezo vya kukopeshwa. Kwa mfano wanaume ambao wamepita umri wa vijana kwa ajili ya kuwawezesha, lakini pia kwenye asilimia 10 zipo baadhi ya halmashauri hazina uwezo kukidhi makundi yote asilimia 10. Ipi kauli ya Wizara hii kuwawezesha makundi hayo ambayo yanabaguliwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mbunge kwa kufatilia kuhusiana na asilimia 10 za fedha zinazotengwa kwenye halmashauri zetu ili kuwasaidia akina mama, vijana na wenyeulemavu katika kufanya biashara zao ndogo ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya mikakati ya Serikali sasa ni kuona makundi haya kwanza yanapata elimu ya ujasiriamali kupitia wataalamu wetu wa Maafisa Biashara katika halmashauri pia kwa kushirikiana na Shirika letu la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) ili waweze kutimiza malengo ambayo wamekusidia katika mikopo hiyo. Lakini zaidi tutaangalia namna ya kuwezesha zile halmashauri ambazo kidogo zina mapato machache ili nao waweze kutosheleza mahitaji katika kuwakopesha vijana na akina mama ambao wanahitaji mikopo kwa ajili ya kufanya biashara zao katika halmashauri zetu na majimbo yetu. Nakushukuru sana.