Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 111 2022-09-21

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini mifuko ya kuwezesha wananchi kiuchumi itaunganishwa ili kuleta tija na manufaa kwa Watanzania hasa waishio vijijini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara inaratibu utekelezaji wa mifuko na programu 62 za uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha tathmini ya mifuko na programu za uwezeshaji ishirini. Napenda kutumia fursa hii kukujulisha kuwa, Serikali inafanyia uchambuzi wa kina taarifa ya tathmini hiyo na kuja na hatua za kuchukua ili kuboresha utoaji wa huduma wa mifuko husika. Nakushukuru sana.