Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza wataalam wa zao la zabibu Dodoma?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nishukuru sana kwa majibu ya Serikali, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza.

Je, Serikali haioni imefikia wakati wa kutenga bajeti maalum ili kuweza kuwapeleka baadhi ya wataalam wa kilimo katika zile nchi ambazo zimekuwa zikizalisha zabibu kwa wingi ikiwemo Afrika ya Kusini, China na Spain? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba tunawajengea uwezo wataalam wetu na hivi sasa tumekamilisha mazungumzo na wenzetu wa Afrika ya Kusini, Ufaransa na Israel kwa ajili ya kuwapeleka wataalam wetu kwenda kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwepo ubunifu na uzalishaji wa mbegu bora na udhibiti wa magonjwa wa wadudu pamoja na mbinu bora za kilimo za shambani yaani agronomy.