Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya ujenzi na ukarabati Vituo vya Afya Chikobe na Bukoli ili vitoe huduma stahiki kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, kwa kuwa hivi sasa halmashauri zimejenga zahanati nyingi na vituo vingi lakini maeneo mengi unakuta anayetibu ni muuguzi badala ya mganga. Ni lini Wizara itafanya tathmini kuona kwamba katika kila zahanati na vituo vya afya kuna idadi ya watumishi wanaotakiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Constantine Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilishafanya tathmini na tunafahamu upungufu wa watumishi katika vituo vyetu na kweli baadhi ya zahanati bado zinahudumiwa na wauguzi bila kuwa na madaktari na waganga. Lakini kama ambavyo Serikali imeendelea kuweka mpango ni kuendelea kuajiri watumishi, mwaka huu watumishi wameajiriwa zaidi ya 7,600 lakini tutaendelea kuajiri kwa awamu ili kuhakikisha watumishi wanapelekwa kwenye zahanati zetu ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya ujenzi na ukarabati Vituo vya Afya Chikobe na Bukoli ili vitoe huduma stahiki kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona, Kituo cha Afya cha Mtanila, pamoja na Kituo cha Afya cha Kata ya Lupa ni vituo vya afya vya muda mrefu na vimechakaa sana. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kukarabati vituo hivi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilifanya tathmini ya vituo vya afya, hospitali na zahanati zote chakavu sana nchini kote na tumeweka mpango wa kuanza kukarabati kwa awamu. Kwa mfano kwa mwaka huu tutakarabati hospitali 19 chakavu za wilaya, lakini tutakwenda pia kukarabati vituo vya afya chakavu na zahanati chakavu kwa awamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya vituo hivyo vya afya.