Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Dar es Salaam Metrpolitan Development Project awamu ya pili utaanza katika Jimbo la Kigamboni?

Supplementary Question 1

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia jibu la Mheshimiwa Waziri, na ni kweli kwamba kero ya barabara ni kubwa sana kwenye Mkoa wa Dar es Salaam na Mheshimiwa Waziri ameahidi maandalizi yataanza januari, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, ni lini hasa ujenzi wa barabara za
DMDP utaanza katika Jiji la Dar es Salaam?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na shukrani zangu za dhati kwa Serikali kwa ujenzi wa barabara lami ya Chanika - Womboza inayoanza kujengwa hivi sasa kero ambayo imeliliwa kwa muda mrefu na diwani wa Kata ya Zigiziwa Mheshimiwa Maige Selemani Maganga.

Naomba kuuliza nini kauli ya Serikali juu ya kutenga fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Dar es Salaam kwa kujenga barabara kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru kwa kunipa fursa lakini nipongeze majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri na ninaomba nijibu mawili ya Mheshimiwa Jerry Silaa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; ni lini Serikali itakamilisha majadiliano na Benki ya Dunia kwa ajili ya kutengeneza barabara Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa miradi hii ni wahakikishie Mheshimiwa Jerry pamoja na Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam tunashirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha negotiations zinaenda haraka iwezekanavyo ili Serikali iweze kufikia makubaliano na Benki ya Dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye nini mwongozo wa Serikali kuhusu mapato ya ndani? Nilishatoa maelekezo kwa halmashauri ambazo zinatenga asilimia 60 ya mapato ya ndani kwa ajili ya maendeleo kutoa asilimia 10 kwa ajili ya kutengeneza barabara za mitaa, ukiwemo Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuwaelekeza wakurugenzi ambao wanahusika na kigezo hiki kuhakikisha asilimia kumi inatengwa na hawatengenezi barabara peke yao wanaungana na TARURA, kuwa na mpango mkakati mmoja ili wanachokitengeneza tuweze kukipima na kupata uhalisia wa matumizi wa fedha. Hayo ndiyo maelekezo ya Serikali. Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri hapo hapo simama, huu mradi wa bonde la Jangwani, fedha zilishatoka, wananchi wamefanyiwa tathmini ya nyumba zao miezi saba iliyopita, mpaka leo kuna sintofahamu, kuna nini huko kwenu? Nasikia mara mnataka mjenge daraja kutoka Magomeni mpaka Mjini?

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, negotiations kati ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa niaba ya Serikali na Benki ya Dunia inaendelea. Lakini kwa sababu Serikali hii nishirikishi na Waheshimiwa Wabunge, kesho mimi, Waziri wa Ujenzi, Waziri wa Fedha na Mipango na pamoja na Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, tuna kikao saa saba kwa ajili ya kujadili jambo hili. Ahsante sana. (Makofi)